MTANGAZAJI

MKUTANO MKUU WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO 2015 WAENDELEA SAN ANTONIO

Baadhi ya Viongozi wa Union 35 zilizopitishwa jana




Mkutano Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani umeingia katika siku ya pili  hii leo ambapo maelfu ya waumini wameendelea kuhudhuria mkutano huo unaofanyika San Antonio Texas huko Marekani.

Mkutano huo ambao ni wa 60 toka kuanzishwa kwa mikutano mikuu ya kanisa hilo ulimwenguni umeanza rasmi hapo jana kwa mapokezi  maalumu wa  Unioni mpya 35 kutoka sehemu mbalimbali duniani ambapo Unioni ya kusini mwa Tanzania,Union ya kaskazini mwa Tanzania na Unioni nne za Divisheni ya Africa Mashariki na Kati ni miongoni mwa union hizo zilizopokelewa.

Katika siku ya kwanza ya mkutano huo umehitimishwa kwa kuchagua kamati ya uchaguzi yenye wajumbe zaidi ya 250 huku Tanzania ikiwakilishwa na Mwenyekiti wa Union ya Kusini mwa Tanzania Magulilo Mwakalonge na Mwenykiti wa Union ya Kaskazin mwa Tanzania Mch Godwin Lekundayo na mshiriki mmoja ambapo mapema hii leo kamati hiyo ilianza kazi yake.

Mkutano mkuu wa kanisa la Wadventista Wa Sabato Ulimwenguni umeanza rasmi hapo jana na unatarajiwa kuhitimishwa Julai 11 mwaka huu kauli mbiu ya mkutano huo ni Inuka uangaze Yesu anakuja.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.