MTANGAZAJI

AMBASSADORS OF CHRIST WAREKODI SANTURI MWONEKANO YA 12




Waimbaji wa Ambassadors Of Christ toka Kigali, Rwanda, juni 5 mwaka huu walifanya tamasha la aina yake katika Chuo Kikuu cha Afrika ya Kati cha Waadventista katika eneo la Gishushu huko Rwanda kwa lengo la kurekodi video ya santuri mwonekano waliyoipa jina la  FATA UMWANA WESE NKU WAWE ambayo imejikita katika kueleza madhara ya madawa ya kulevya kwa vijana katika jamii.

.Toleo hilo lenye nyimbo za Kinyarwanda ni la 12 toka waimbaji hao waanze kuimba mwaka 1995, kwa lengo la kutangaza injili na kuwaunganisha wanyarwanda baada ya mauaji ya kimbali ya mwaka 1994.

Waimbaji wengine walioshiriki kwenye tamasha la kurekodi video ya santuri hiyo ni Shalom, Friends of Jesus, Paradise Melody, Epedusalut, Patmos, Maranatha Men, Maranatha Family na Orion Singers.

 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.