MTANGAZAJI

UPENDO NKONE, MIKE KALAMBAY WANOGESHA TAMASHA LA GOSPEL COLUMBUS, OHIO


Mwimbaji wa nyimbo za injili wa Columbus, Ohio Enock Mwamba(kati) akiimba moja ya nyimbo za injili huku akiwashirikisha Mike Kalambay aliyekuja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Upendo Nkone aliyekuja toka Tanzania maalum kunogesha tamasha la Gospel lililofanyika siku Jumapili May 24, 2015 na kuhitimisha tamasha hilo lililokua la siku 3 mjini humo lililoanzia siku ya Ijumaa May 22, 2015.
Mike Kalambay akiimba huku akitoa neno la Mungu kwa Kifaransa kilichochanganyika na lingala huku mchungaji Fayes (kulia) akitafsiri kwa kiingereza na Kiswahili.
Mike Kalambay akiimba moja ya nyimbo za injili kwenye tamasha la gospel lililofanyika siku ya Jumapili May 24, 2015 mjini Columbus, Ohio.
Mike Kalambay toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo akishambulia jukwaa na nyimbo za injili.
Mwimbaji mahili wa nyimbo za Injili Upendo Nkone akiimba moja ya nyimbo zake kwenye tamasha hilo.
Upendo Nkone na mchungaji Donis Nkone wakifuatilia tamasha Mike Kalambay (hayupo pichani).
Mchungaji Donis Nkone na mke wake Nnunu Nkone wakiwa wamepiga magoti wakati Mike Kalambay akiwashukuru kwa kufanikisha ujio wake ikiwa ndio mara ya kwanza kwa yeye kufika mjini humo.
Mike Kalambay(kati) akipata picha ya pamoja na mchungaji Donis Nkone na mkewe Nnunu Nkone mara tu baada ya kumalizika kwa tamasha hilo lililovuta watu mbalimbali wa mataifa tofauti mjini Columbus, Ohio.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.