MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:WAJUMBE WA TUZO YA JAMII WATEMBELEA UKUMBI KUTAKAKOFANYIKA UTOAJI WA TUZO HIYO MWAKA HUU

Ndani ya Ukumbi kutakakofanyika hafla ya utoaji wa Tuzo ya Jamii



Wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya Tuzo ya Jamii ndani ya ukumbi.




Katibu wa Tuzo ya Jamii Amani Theophilas Mwaipaja akisisitiza jambo

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tuzo ya Jamii DJ Malegesi akiwa na Mhandisi Sylvester Mayunga (Mjumbe)
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Tuzo ya Jamii itayotolewa Aprili 13 mwaka huu wametembelea katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC) ambako kutafanyika hafla ya utoaji wa Tuzo hiyo.

Tuzo hiyo iliyoandaliwa na  Kampuni ya Tanzania Awards International Limited itakuwa katika kipengele cha  Tuzo ya Jamii ya heshima itakayotolewa kwa Rais wa awamu ya kwanza wa  Tanzania Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa kwanza wa Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela.


Pamoja na Tuzo hiyo ya heshima pia itatolewa Tuzo ya Haki za binadamu ambapo mshindi atatangazwa siku hiyo, Tuzo kwa  mwanasiasa kijana na mwanasiasa mtu mzima  mwenye mafanikio katika siasa za Tanzania.


Washindi wa siasa  watapatikana baada ya kupigiwa kura kupitia huduma ya simu ya mkononi ya PUSH ambapo  vigezo vya kutazama unapopiga kura kuwa ni pamoja na  uvumilivu katika siasa ,uwezo wa kuibua na kutetea hoja ,ushiriki wake katika kutetea maslahi ya Taifa,ushiriki wake katika huduma za Jamii na Nidhamu katika shughuli zasiasa. 


Hii itakuwa ni mara ya Kwanza nchini Tanzania kwa Kampuni ya Tanzania Awards Internation Limited kutoa Tuzo ya Heshima kwa viongozi hao huku mgeni rasmi katika hafla hiyo akitarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Jakaya Mrisho Kikwete.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.