MTANGAZAJI

ARUSHA:CHUO KIKUU CHA ARUSHA CHAELEZA ALIYOYAFANYA MCHUNGAJI NICANOR KIKIWA WAKATI AKIWA MWANAFUNZI CHUONI HAPO




 


 Marehemu Mchungaji Nikanor Kikiwa (Pichani) aliyefikwa na mauti Februari  17,2015  katika hospitari ya Dar Group amezikwa leo huko Morogoro.

Nikanor aliyezaliwa mwaka 1980 alijiunga na Chuo Kikuu cha Arusha  Januari 8,2004 na kuhitimu masomo yake ya shahada ya kwanza  ya Thiolojia Julai 2,2007.


Akiwa anasoma katika  Chuo kikuu cha Arusha marehemu Nikanor Kikiwa alijituma sana kwenye masomo na kuonyesha juhudi kubwa ya  mambo ya kiroho na ushirikiano mzuri na wanafunzi wenzake, waalimu na jamii nzima kwa ujumla.


1.Marehemu Mch Nikanor Kikiwa aliwahi kuwa mmoja wa viongozi wa  chama cha wachungaji Chuo Kikuu cha Arusha yaani University of Arusha Ministeral Association na kupitia uongozi wake,wachungaji waliokuwa wanasoma kipindi hicho walisaidia wanachuo wengine kuwa na maadili mema chuoni hapo.


2.Alikuwa mwimbaji katika vikundi vya  Harvest Brothers,Pilgrims na Early Melodies vilivyoboresha program mbalimbali za kiroho  na kukitangaza Chuo.


3.Alikuwa mtanashati jambo ambalo lilisababisha  wanafunzi wenzake kuguswa na kubadilika nakuwa watanashati.


4.Aliuanza uchungaji wake hata kabla hajamaliza masomo kwani akiwa chuokikuu cha Arusha alitumia muda wa jioni kushauri wanafunzi wenzake na kutembelea washiriki na wasio washiriki kwalengo la uinjilisti(Ucheshi ulimuwezesha kuwa na marafiki wengi).


5.Alijituma sana katika programu za vijana na alifanya kwa vitendo kile alichokuwa anakifanya Darasani jambo ambalo lilisaidia Chuo Kikuu cha Arusha  kuwa na timu ya Masterguide nzuri kipindi chake akiwa chuoni.


6.Alikuwa na Ujasiri muwazi hakuogopa kuitaja dhambi kwa jina alipoona wanafuzi wenzake wanakosea aliwaendea nakuwaambia hapo umekosea hili halikuishia kwa wanafunzi wenzake tuu hata kwa wakufunzi Alikuwa mtu wa Kiroho.


Chuo Kimempoteza ALUMNI wake ambaye alikuwa mstari wa mbele kutoa mawazo ya namna ya kuboresha Chuo kikuu cha Arusha .

Imetolewa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma wa Chuo Kikuu cha Arusha 


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.