MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:KONGAMANO LA TAIFA LA WATOTO WANAOISHI NA VVU/UKIMWI KUFANYIKA KESHO



Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Shirika la huduma za watoto la Elizabeth Glaser Pediatric Foundation (EGPAF),UNICEF na wabia wengine wa huduma za Virusi vya UKIMWI (VVU) pamoja na Chama cha Madaktari wa watoto Tanzania (PAT) imeandaa kongamano la nne la Taifa la watoto wanaoishi na VVU/ UKIMWI.
Akizungumza na waandishi wa habari jiji Dar es salaam mapema leo, Mratibu wa huduma za UKIMWI kwa watoto Dr Aneth Rwebembera  amesema kuwa kongamano hilo linatarajia kufanyika tarehe 19 na 20 Nov 2014 katika kituo cha mikutano ya kimataifa cha Mwl Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
Ameongeza kuwa kauli mbiu ya kongamano hilo ‘’Kuongeza Kasi’’ Ikiwa ni kuimarisha upatikanaji wa huduma,vipimo, matunzo na tiba ya VVU ili kuboresha maisha ya mtoto.
Kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali wakiwemo washiriki wa kitaifa na kimataifa wanaojihusisha na  udhibiti wa VVU kwa watoto,wawakilishi kutoka Wizara za serikali, wabia wa maendeleo na mashirika mengine,huku lengo ni kuongeza uelewa wa taifa wa mikakati mipya ya utoaji huduma ya kudhibiti VVU na kuuelimisha umma kuhusu hali ya sasa kuhusianan na huduma za VVU/UKIMWI kwa watoto.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.