MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:KAMATI KUU YA UTENDAJI YA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO KUSINI MWA TANZANIA YAFANYA KIKAO CHAKE

Kamati kuu ya utendaji kazi ya kanisa la Waadventista Wasabato Union ya Kaskazini mwa Tanzania imezindua kikao chake cha pili cha mwisho wa mwaka mapema hii leo katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato mwenge jijini Dar es salaam.

Katibu wa Mkuu wa  Union ya Kusini mwa Tanzania Mch James  Machage amesema kuwa lengo kuu la kikao hicho ni kutoa ripoti za utendaji kazi wa idara zote zilizopo ndani ya union ya kusin mwa Tanzania. 

Mchungaji James Machage ameongeza kuwa kikao hicho pia kinalenga mipango na mikakati ya kazi ya injili kwa mwaka 2015.

Aidha Mchungaji Machage ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam kuhudhuria katika kanisa la Waadventista Wa Sabato Mwenge siku ya kesho saa mbili asubuhi kwa ajili kusikiliza taarifa za utendaji kazi wa idara mbalimba zilizopo ndani ya kanisa.

Kikao hicho kilichozinduliwa hii leo kinatarajia kuendelea mapema kesho asubuhi kikihudhuriwa na viongozi wote wa Union ya Kusini mwa Tanzania viongozi wote wa majimbo ya mashariki mwa Tanzania na jimbo la nyanda za juu za kusini pamoja na viongozi wa idara mbalimbali pia kikihudhuriwa na viongozi toka Division ya Afrika Mashariki na Kati.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.