MTANGAZAJI

MANYARA:JAMII YATAKIWA KUHESHIMU NDOA



 

Mkurugenzi wa Idara ya huduma za wanawake,watoto na shule ya Sabato Konferensi ya Nyanza Kusini ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Bi Esther Malyeta (Pichani) ameitaka  jamii kuziheshimu ndoa ili kujenga kizazi bora cha leo na baadae .

Akihutubia mamia ya wakazi wa mji wa Haydom Mkoani Manyara jana jioni Bi Malyeta ambaye aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Hanang na Sengerema  amesema kuwa familia nyingi zimesambaratika kutokana na kukosekana kwa  upendo na huruma ndani ya ndoa.

Bi Malyeta amesema kuwa kama ndoa hazitaheshimiwa watoto wa waishio katika mazingira magumu hawatapungua kamwe,kwa kuwa watoto wengi walioko waishio katika mazingira magumu sio kwamba hawana wazazi bali wazazi wao wamefarakana hivyo imewalazimu kutawanyika kuhitaji msaada wa kuishi.

Ameeleza kuwa inashangaza kuona mume anampiga mke wake hali kadhalika mke kumpiga mume wake kwani Biblia inaeleza kuwa mume na mke ni mwili mmoja sasa yawezekanaje mtu kujipiga mwenyewe.

 Nao wakazi wa Mji wa Haydom wamesema kuwa uwepo wa mkutano wa injili unaoendeshwa na Idara ya wanawake wa Unioni konferensi ya kaskazini mwa Tanzania katika viwanja vya CCM mjini Haydom utaibadilisha jamii kumwelekea mungu kupitia mafundisho mbalimbali yahusuyo wokovu na maadili mema ambao wa kwanza kuwepo mahali kwenye eneo hilo tangu kanisa la waadventista wasabato lilipojengwa na kusimikwa mjini humo.

Mkutano huo ulianza siku ya Jumapili kwa ufunguzi rasmi uliofanywa na diwani wa kata ya Haydom mheshimiwa  Nathanieli Nasasu utahitimishwa Novemba 2,2014.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.