MTANGAZAJI

IDADI NDOGO YA WASHIRIKI WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO YAONGEZEKA KATIKA KIPINDI CHA MIEZI 10 NCHINI



Idadi ya washiriki wa kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Tanzania imeonekana kuwa na idadi ndogo iliyoongezeka katika kipindi cha miezi  10 iliyopita.

Takwimu zilizotolewa mwaka huu na makao makuu ya kanisa hilo katika maeneo yake mawili ya kiutendaji hapa Tanzania yaani Unioni Konferensi ya Kaskazini na Unioni ya Kusini zinaonesha kuwa Unioni ya Kaskazini yenye konferensi nne mpaka kufikia mwishoni mwa robo ya pili ya mwaka 2014 ilikuwa na washiriki 336,305 na ile ya kusini yenye konferensi mbili ina washiriki 104,348.

Hii inamaanisha kwamba kuna washiriki wa kanisa hilo kwa sasa wapatao 440,653 kati ya watanzania zaidi ya milioni 40 kwa mujibu wa takwimu hizo ambalo ni ongezeko  la washiriki 29,362 katika  kipindi cha miezi 10 toka disemba mwaka jana.

Takwimu zilizotolewa na Uongozi wa Kanisa hilo  Disemba  mwaka jana zinaonesha kulikuwa na washiriki wa kanisa hilo wapatao 322,351 katika Unioni Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania na washiriki 88,940 katika Unioni ya kusini mwa Tanzania hii ni kwa mujibu wa Takwimu zilizotolewa na uongozi wa kanisa hilo nchini.

Hata hivyo utafiti unaonesha kuwa makanisa mahalia yamekuwa yakishindwa  kutoa malezi ya kiroho na kuratibu idadi kubwa ya washiriki wapya wanaoongezeka kutokana na mikutano mbalimbali ya injili inayofanyika nchini ambapo jumla ya watu 35,657 walibatizwa katika kanisa hilo katika kipindi cha mwezi Januari hadi Septemba mwaka jana na hivi karibuni huko jijini mwanza walibatizwa watu 3000

Kanisa la Waadventista Wa Sabato duniani lina waumini milioni 18 katika nchi 215 zilizopo kwenye  divisheni 13 za kanisa hilo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.