MTANGAZAJI

LHRC-YAWAOMBA WANANCHI WA TANZANIA KUUNGA MKONO KUPINGA ADHABU YA KIFO



Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini kimewaomba wananchi kuunga mkono jitihada za kituo hicho katika kupinga adhabu ya kifo kwani adhabu hiyo inakwenda kinyume na haki za binaadam lakini pia kuvunja sheria ya haki ya mtu ya kuishi.

Akizungumza na Morning Star Radio katika kipindi cha Jamii yetu jana , Mwanasheria kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binaadam Bi. Benadetha Thomas amesema kuwa, kituo cha sheria na haki za binadamu kinapinga adhabu ya kifo kwasababu wakati mwingine mtuhumiwa anakuwa hajafanya kosa hilo na inapogundulika tayari hukumu ya kifo inakua imeshatekelezwa.

Mwanasheria huyo amesema kwa kipindi chote cha awamu mbili za Rais wa awamu ya tatu na awamu ya nne haijawahi kutekelezwa ingawa tayari hukumu za adhabu ya kifo zimeshatolewa na wafungwa zaidi ya 364 wapo kwenye magereza mbali mbali nchini lakini hawajui lini hukumu zao zitatekelezwa.

Thomas ameyasema hayo ikiwa zimebaki siku 4 ili kuweza kuadhimisha siku ya kupinga adhabu ya kifo duniani ambayo hufanyika October 10 kila mwaka, huku kituo cha sheria na haki za binaadamu kikijipanga kwa ajili ya kutoa Tamko  ili kupinga adhabu hiyo hapa nchini.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.