MTANGAZAJI

KAGERA:MWANAFUNZI WA DARASA LA TANO AJINYONGA



Mwanafunzi wa Darasa la tano katika Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihugo Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera, Ezra Gerald  amejinyonga hadi kufa kwa kutumia shuka ya hospitali, alikokuwa amelazwa kwa kile kinachosemekana alikuwa anasumbuliwa na homa ya tumbo.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera Gilles Muroto amethibitisha kutokea kwa tukio hilo nakuongeza kuwa mapema juma hili majira ya  asubuhi waliukuta mwalimu wa marehemu ukiwa kwenye mti nje ya hospitali aliyokuwa amelazwa,huku kukiwa na ujumbe unaonyesha amechukua uamuzi huo, kutokana na kuchukizwa na uamuzi wa daktari aliyemhudumia wa kumlaza ili atibiwe ugonjwa ambao hakua anaumwa.

Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo imekuwa ikihusishwa na matukio mbalimbali ya kutisha,ambapo Agasti 8 mwaka huu Watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walivamia na kuwaua mume na mke na kumjeruhi mtoto mchanga mwenye umri wa miezi 4 .

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.