UHARIBU WA MAZINGIRA HUENDA UKAKOSESHA MAJI WAKAZI MJI WA MTWARA
Wakazi wa mji wa mtwara wako hatarini kukosa huduma ya maji baada ya watu wasiofahamika
kuvamia na kuchimba mchanga kwenye chanzo cha maji katika kijiji cha Namayanga
kata ya ziwani .
Taarifa zinasema kuwa kutokana na shughuli hizo za uchimbaji
mchanga kushamiri maji yamehama kwenye mkondo wake khali inayopelekea wakazi wa
maeneo hayo kukosa huduma hiyo muhimu.
Aidha kutokana na na uharibifu huo kumelazimu Mkuu wa Wilaya
ya Mtwara Wilman Ndile kupiga marufuku uchimbaji wa mchanga katika eneo hilo
Asilimia 99 ya wakazi
wa Mtwara wanategemea kupata maji kutoka katika vyanzo hivyo na iwapo
wachimbaji wataendelea na zoezi hilo basi biashara hiyo itasababisha shida
kubwa ya upatikanajji wa maji katika
maeneo hayo.
Akitoa taarifa kwa mkuu wa wilaya kaimu mkurugenzi wa
mamlaka ya maji Mtwara (MTUWASA)Ndugu Kubiri Masunga amesema uharibifu huo ulianza siku nyingi na kwamba pamoja na
hatua kadhaa kuchukuliwa ili kuzuia uhalibifu huo lakini bado watu wamekuwa wakiendelea na uchimbaji
huo.
Post a Comment