MTANGAZAJI

UHAMIAJI:WAHAMIAJI HARAMU 400 WALIKAMATWA NGARA JANUARI HADI APRIL 2014



Wahamiaji haramu wapatao 400 raia wa Burundi wamekamatwa na idara ya uhamiaji  wilayani Ngara mkoani Kagera kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria na kurejeshwa makwao katika Kipindi maalum cha oparesheni kimbunga iliyofanyika katika mikoa ya kanda ya Ziwa Victoria.

Ofisa wa idara ya uhamiaji wilayani ngara ndugu Marwa Kitang’ita amesema wahamiaji hao walikamatwa katika msako maalum kwenye vijiji vya tarafa ya Rulenge,Kanazi na Nyamiaga  kuanzia January hadi april mwaka huu

Kitang’ita amesema  wananchi wa vijiji vya vilivyoko mpakani mwa nchi jirani za Rwanda na Burundi wanachangia kwa kiasi kikubwa kuwakaribisha wahamiaji hao na kuwafanyia shughuli mbalimbali ikiwemo  kuwachungia mifugo.

Amesema katika msako huo bado viongozi wa vitongoji na vijiji hawatoi ushirikiano wa dhati ili kuwabaini wahamiaji badala yake wamekuwa  wakilalamikia wanapoutana na uhalifu hasa wanapoibiwa  mali zao.

Pamoja na oparesheni kimbunga kufanyika katika mikoa ya geita Kagera na kigoma bado wahamiaji wanarejea kwa kisingizio cha kuendeleza mashamba waliopewa ama kununua kutoka kwa watanzania .

Kitang’ita ameongeza kuwa changamoto kubwa inayokabili idara ya uhamiaji Ngara ni ukosefu wa vitendea kazi hasa magari na mafuta ya vyombo vya usafiri na hivyo kusababisha baadhi ya maeneo yaliyoko mbali kutofikika kwa haraka . wanaoingia katika madaftari ya mabalozi na wenyeviti ili kukabailiana na wimbi hilo la wahamiaji haramu.

Mkuu wa wilaya ya ngara Costantine kanyasu amewataka viongozi wa vijiji na mitaa kuorodhesha wageni wanaoingia katika madaftari ya mabalozi na wenyeviti ili kukabailiana na tatizo hilo

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.