MTANGAZAJI

CAG ASEMA PRIDE TANZANIA SI MALI YA SERIKALI



Taasisi ya Pride Tanzania ambayo hutoa mikopo midogo midogo kwa wajasiriamali  imetoweka kwenye orodha ya mali zinazomilikiwa na serikali.

Taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu  wa hesabu za serikali CAG Inasema taasisi hiyo ilianzishwa mei mwaka 1993 chini ya sheria ya mahakama.

Amesema dhumuni la kuanzishwa taasisi hiyo ni kutoa mikopo midogo midogo kwa wajasriamali nchini.

CAG amesema  taarifa za msajili wa hazina inaonesha kuwa uwekezaji wa serikali katika kampuni kufikia juni 30  mwaka 2008 hisa zote za Pride zinamilikiwa na serikali .

Taarifa hiyo inasema mtaji hadi juni 30  mwaka 2008 unaonesha kuwa ni Shilingi za kitanzania 2.301 bilioni ,na fedha za wanahisa wengine  zilikuwa ni jumla ya shilingi 2.198 bilioni, na hivyo kuufanya mtaji mzima kuwa shilingi 4.499 bilioni.

Kwa mujibu wa taarifa ya masajili wa hazina iliyoishia juni 30 mwaka jana shirika hilo halipo tena kwenye moja ya mashirika ya umma.

Hata hivyo amesema kuwa uhalali na sababu za kuondolewa kwa shirika hilo katika orodha ya msajili  wa kampuni hazikufahamika.

Kwa mujibu wa  sheria ya ukaguzi wa umma namba 11 ya mwaka 2008 kila shirika la umma linatakiwa kupeleka hesabu kwa CAG Kukaguliwa katika kipindi cha miezi 3 baada ya mwaka wa fedha kukamilika .

Hata hivyo hesabu za pride Tanzania hazijawahi kuwasilishwa kwa CAG kama inavyotakiwa kisheria jambo linaloibua maswali kwa jamii.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.