MTANGAZAJI

TABORA:JESHI LA POLISI LAKAMATA WANNE KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA SIRAHA NA SARE ZA JESHI



Jeshi la polisi mkoani Tabora linawashikilia watu wanane kwa tuhuma za makosa mbalimbali,ikiwamo ya umiliki wa silaha kinyume cha sheria na kukutwa na sare za Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Kamanda wa polisi mkoani Tabora Susan Kaganda amesema kuwa matukio hayo yametokea maeneo tofauti na watuhumiwa wamekamatwa kwenye operesheni ya kukabiliana na uhalifu.

Kaganda amedai kuwa katika tukio la kwanza la kukamatwa mkazi wa Inyonga akiwa na Risasi 307 za Bunduki aina ya SMG,mtuhumiwa alikiri kujihusisha na uchuuzi wa risasi na matukio mbalimbali ya unyang`anyi wa kutumia silaha .

Jeshi la polisi  nchini Tanzania  linatoa wito kwa raia wote kushirikiana na jeshi hilo ikiwemo kutoa taarifa za kuwabaini wahalifu katika lengo la kukomesha vitendo vya kihalifu nchini humo.



No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.