MTANGAZAJI

KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO MZIZIMA LASAIDIA WATU WASIOJIWEZA



Chama  ya kinachowaunganisha wanaume na wanawake wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato AMO DORKAS katika kanisa la Waadventista Wa Sabato Mzizima jijini Dar es salaam wametembelea kituo cha watu wasiojiweza cha Nunge kilichoko jijini Dar es salaam na kutoa misaada ya kijamii na kiroho.  



Kituo hicho ambacho  kipo chini ya Serikali kina idadi ya wazee 37, watoto wanaoishi na ulemavu wa kusikia 23  na watoto yatima.



Sambamba na kutoa huduma ya neno la MUNGU  pia wametoa  msaada wa mavazi,mchele, sabuni,  na unga wa lishe na dawa kwa Wagonjwa.



Kwa upande wake   kiongozi wa mawasiliano wa kanisa la mzizima Kapesa Manyoni  ambaye pia alikuwa mkuu wa msafara ameiomba jamii kuonesha upendo kwa watu wasiojiweza na kwamba wao kama kanisa wataendelea kufanya hivyo.



Kwa  upande wake Afisa Msaidizi wa Kituo hicho Bwana Mosses Gunza ameshukuru kwa kupokea  msaada huo na kusema kuwa ni kuonesha upendo wa Mungu kwa watu wasiojiweza kwani Hawakupenda kuwa hivyo.



Wazee hao pamoja na watoto yatima wameiomba serikali kuweka utaratibu wa kuwahisha misaada  ili iweze kuwafikia kwa wakati  hali ambayo itasaidia upatikanaji wa mahitaji kwa urahisi.

               




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.