MTANGAZAJI

AJAAT YATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI KUHUSU HARAKATI ZA KUJILINDA DHIDI YA VVU NA ATHARI ZA UKIMWI

Mratibu wa UNAIDS nchini Tanzania Dr Patrick Brenny akifungua mafunzo



Chama Cha Waandishi wa Habari Dhidi ya UKIMWI Tanzania (AJAAT) kimefanya mafunzo kwa ajili ya waandishi wa habari Dar es salaam
.

Mafunzo hayo yaliyodhaminiwa na Shirika la Kimataifa Kuhusu Masuala ya UKIMWI la UNAIDS Tawi la Tanzania (UNAIDS-Tanzania) yanalenga kuwaelimisha waandishi wa habari mbinu bora za  jinsi ya kupiga vita Unyanyapaa na Ubaguzi unaohusiana na VVU/UKIMWI kwa kutumia taaluma yao.


Aidha mafunzo haya pia yatatoa mwanya wa kufanya tathmini ya mchango wa vyombo vya habari katika harakati za kutokomeza maambukizi ya VVU na katika kupambana na athari za UKIMWI, kubadilishana mawazo na uzoefu na wadau walio katika harakati hizo na kuweka mikakati ya pamoja katika kufanikisha azma hiyo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.