MTANGAZAJI

ZAWADI YA KUREKODI ALBUM BURE KWA WAIMBAJI WA INJILI TOKA KWA MTANGAZAJI HII HAPA


Kampuni ya Excellent Pro ya jijini Dar es salaam kwa kushirikiana na kipindi cha Lulu za Injili na Acappella vya Morning Star Radio wanakuletea zawadi mwimbaji/waimbaji wa nyimbo za injili zawadi nyingine mwaka huu wa 2013 yaani GOSPEL OFFER MWAKA 2013.


· Lengo la Gospel offer 2013 ni kuchangia/kusupport juhudi zinazofanywa na wasanii (Kwaya za kanisa, Vikundi binafsi na Mwimbaji mmoja mmoja) katika kutambua vipaji.

·    Gospel Offer 2013 inadhaniniwa na kipindi cha Lulu za Injili na Acappella kwa kushirikiana na Excellent Pro.
·         Gospel Offer 2013 inadhamilia kurekodi albam 1 ya nyimbo mpaka 12 kwa kwaya na 10 kwa vikundi na mwimbaji binafsi.
·         Kumbuka kuwa  Gospel offer ya 2012  ilimpatia zawadi Angel Magotti kurekodi wimbo mmoja bure


·  Makundi yanayokusudiwa kuingia katika mchakato wa kupata mshindi katika Gospel offer 2013 ni kwaya za kanisa, vikundi na mwimbaji binafsi.
·  Kwaya, vikundi au mwimbaji binafsi atagharimiwa gharama za kurekodi  katika mojawapo ya studio zilizopo Dar es salaam. Usafiri, chakula na gharama zingine ni wajibu wa kwaya, kikundi au mwimbaji binafsi.
·    Mchakato wa kumpata mshindi atakayenufaika na Gospel Offer 2013 utachukuwa mwezi mmoja; na tukio la kurekodi litakuwa mwezi wa tisa 2013, ili kutoa muda muafaka kwa maandalizi ya mshindi kufanya vizuri.

VIGEZO (CRITERIA)

·         Ni kwaya, vikundi na waimbaji binafsi wa nyimbo za injili tu.

·         Kwaya, vikundi na waimbaji binafsi ambao watakuwa na mipango madhubuti ya kufanya recording tu.  Mchakato wa kuchuja utawaengua ambao hawatakuwa na dhamira za dhati kurekodi.

·         Kwaya, vikundi au waimbaji binafsi wanaoibuka watapata kipaumbele.

·         Mshindi atapatikana kwa kupigiwa kura nyingi na wasikilizaji wa kipindi cha Lulu za injili.

·         Mwakilishi/mhusika wa kwaya, kikundi au mwimbaji binafsi yoyote ana nafasi ya kupendekeza jina la kwaya, kikundi au mwimbaji binafsi.

        


NAMNA YA KUSHIRIKI
·         Pendekeza jina la kwaya, kikundi au mwimbaji binafsi tuma ujumbe wa simu GO……….kwenda namba 15551………….

·         Pigia kura kwaya unayopenda kuwa mshindi wa Gospel offer 2013 tuma ujumbe wa simu GO…. Kwenda namba 15551………….


RATIBA YA MCHAKATO WA KUPATA MSHINDI
·         ( July 7 – 13, 2013) – Kuzindua Gospel Offer 2013

·         (Julai 14 – 20, 2013) – Majina ya Kwaya, vikundi na waimbaji binafsi kupendekezwa kwa ujumbe wa simu.

·         (Julai 21 – 27, 2013) – Kuchuja kwaya zibaki 5, vikundi 2 na waimbaji binafsi 2 na kuwatangaza.

·         ( Julai 28 – Agasti 3, 2013) – Wasikilizaji wa Lulu za injili/Acappella kupiga kura kwa ujumbe wa simu.

·         (Agasti 4 – 10, 2013) Wasikilizaji wa Lulu za injili/Acappella kupiga kura kwa ujumbe wa simu.

·         (Agasti 11 – 17, 2013) kufanya tathimini ya kura za wasikilizaji wa Lulu za injili /Acappella kutangaza washindi wawili (Kwaya moja na Kikundi/mwimbaji binafsi)

·         (Agasti 17 – 31, 2013) Washindi kujiandaa na mazoezi kwa ajili ya kurekodi.

·         Septemba 1, 2013 – Kwaya kurekodi

·         Septemba 8, 2013 – Kikundi/au mwimbaji binafsi kurekodi

·         Septemba 9 – 14, 2013 Kazi ya kwaya mshindi kutamburishwa

·         September 15 – 21, 2013 Kazi ya kikundi/mwimbaji binafsi kutambulishwa

·         Septemba 22 – 28, 2013 Kuwapa pongezi washindi katika vipindi vya Lulu za injili/Acappella




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.