MTANGAZAJI

KANISA LA WASABATO LATOA MATIBABU BURE ZANZIBAR

Baadhi ya Wananchi wakisubiri matibabu ya bure katika kituo cha Afya cha Meya cha Kanisa la Waadventista Wasabato

Mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mheshimiwa Sultan Muhamed Mugheir wengine ni Mkurugenzi wa idaya ya afya kanisa la wasabato Tanzania Dr Geogfrey Mabuba(kulia),kushoto ni Meneja wa kituo cha Afya Mchungaji Bunga Detu


Baadhi ya wahudumu wa afya wakitoa madawa kwa wakazi wa Zanzibar

Dr Peter Omwanzi akiwa na madawa mbalimbali yaliyotolewa



Baadhi ya wakazi wa Zanzibar wakisubiri kupata matibabu hayo

Kanisa la Waadventista Wasabato nchini Tanzania limetoa matibabu bure kwa wananchi wa Zanzibar kupita kituo chache cha afya kilichopo Meya,Zanzibar.

Akizungumza na blog hii Mkurugenzi wa idara ya Afya katika kanisa hilo kanda ya mashariki mwa Tanzania Dr Livingstone Kingu amesema zaidi ya shilingi milioni 4 za kitanzania zilitumika kununulia madawa kwa ajili ya matibabu hayo yaliyofanyika kwa muda wa siku 3

Matibabu hayo yaliwahusisha wananchi wapatao 2700 kati yao watu 500 walipatiwa miwani baada ya kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya macho

1 comment

Anonymous said...

Inatia moyo!

Mtazamo News . Powered by Blogger.