MTANGAZAJI

UMOJA WA WATANZANIA UJERUMANI (UTU e.V ) UMEFANYA MKUTANO MKUU NA KUCHAGUA VIONGOZI




Umoja wa Watanzania Ujerumani UTU e.V umefanya  mkutano mkuu wa uchaguzi mjini Aschaffenburg Ujerumani jumamosi 28.09.19. 

 Katika uchaguzi huo watanzania wanaoishi Ujerumani walichagua viongozi wapya, nafasi ya Mwenyekiti alichaguliwa Mwl. Bi Upendo Vanessa Lyimo kuwa Mwenyekiti wa UTU e.V,  baada ya mwenyekiti mstaafu Bw. Mfundo Peter Mfundo kukataa kugombea nafasi hiyo, ambaye amekaa kwa muda wa miaka 9, na kukitumikia chama hicho kwa muda wote huo, hata hivyo kamati ilimuomba achukue nafasi ya heshima kuwa mwanakamati, mshauri, mlezi wa UTU e.V na Kiongozi Mwandamizi katika shughuli za UTU e.V

Watanzania wanaoishi Ujerumani waliwachagua  viongozi wafuatao.
Mwenyekiti: Mwl. Bi Upendo Vanessa Lyimo
Makamo Mwenyekiti:  Bw. Malumbo Salim Malumbo 
Katibu:  Bi.  Petrida Karch
Muweka Hazina: Bw. Mngoya Lukuta

Wanakamati:
Bw. Mfundo Peter Mfundo  
Bw. Ebrahim Makunja (aka Kamanda Ras Makunja)
Bw. Sudi Mnette

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.