MTANGAZAJI

EMIRATES WAANZA KUHAKIKI TAARIFA ZA WASAFIRI KWA TEKNOLOJIA YA UTAMBUZI WA SURA




Shirika la Ndege la Emirates limeanza kutumia Teknolojia ya utambuzi wa sura (Facial Recognition) katika kuhakiki taarifa za wasafiri wanaotumia ndege hizo,jambo linaloelezwa kuwa litaokoa  muda wakati wa ukaguzi kwenye viwanja vya Ndege. 


Kupitia mtandao wa Twitter wa Emirates wameeleza kuwa shirika hilo limekuwa la kwanza kutumia  huduma hiyo kwa wasafari wanaotumia Ndege zake wanaotokea Marekani na Dubai na hiyo kulifanya kuwa shirika  la kwanza nje ya Marekani kuthibitisha taarifa za mteja kwa teknolojia ya kutambua sura baada ya Marekani kuruhusu matumizi ya teknolojia hiyo kupitia kitengo cha udhibiti cha CBP (Customs Border Protection).

Teknolojia ya “Biometric boarding” ilitumika kwa mara kwanza kwa wateja ambao waliondoka Dubai kuelekea jiji la New York nchini Marekani siku chache zilizopita ambapo Emirate walieleza kuwa teknolojia hiyo ilifanikiwa kutumika kwa kuwahudumia wateja kwa utambuzi wa sura  kwa asilimia 100. 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.