MTANGAZAJI

RIPOTI MAALUM: MABADILIKO YA TABIANCHI YAATHIRI VISIWA VYA MAFIA NCHINI TANZANIA

DSC_2410
Moja ya eneo lililoaribika kutokana na hali ya mabadiliko ya tabianchi (Climate Change) katika fukwe ya Kilindoni, katika Kisiwa cha Mafia, Mkoani Pwani, nchini Tanzania. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog). 

Kisiwa cha Mafia kijiografia kipo karibu na mlango wa Mto Rufiji kusini mwa Tanzania.

Hata hivyo, Kisiwa hicho ambacho ni Wilaya moja wapo ya Mkoa wa Pwani inakabiriwa kwa kiwango kikubwa na changamoto za Mabadiliko ya tabianchi hasa baada ya wananchi wake wengi kutopata elimu hiyo sahihi.

Imeelezwa kuwa, elimu juu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi katika Kisiwa cha Mafia ambacho pia kinaunda visiwa vidogovidogo zaidi ya vitano, wananchi walio wengi katika kisiwa hicho bado hawajapata elimu sahihi ya kukabiliana na mabadiliko ya kimazingira (Climate Change).

Mtandao huu ambao ulipiga hodi katika kisiwa hicho cha Mafia ili kupata habari za mabadiliko ya tabianchi na namna ya Mabadiliko ya tabianchi yanavyo athiri Kisiwa hicho (How Climate Change effects Mafia Island in Tanzania) ambapo iliweza kuzungumza na maafisa Ardhi, Mazingira  na wananchi wa Wilaya hiyo,  na kueleza haya:

Kwa upande wa Afisa Mazingira wa Wilaya hiyo, Gideon  Zakayo  amebainisha kuwa, Kisiwa cha Mafia kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za Kimazingira ikiwemo hali ya Mabadiliko ya tabianchi huku suala la elimu kwa wananchi likiwa dogo kutokana na kutokuwa na fungu la kutosha.

Zakayo ameongeza kuwa, Suala la Mazingira ni pana kwani limejumuisha Afya, Maji, Kilimo, Misitu, ardhi na mazingira yote kwa ujumla hivyo wadau wanahitajika kujitokeza kusaidiana na Serikali katika kutoa elimu, kuelimisha sera na taratibu zinazotakiwa kufuatwa na wananchi katika maeneo husika.

Aidha, ameongeza kuwa, katika miongoni mwa visiwa vidogo vidogo ndani ya Mafia, kuna baadhi ya visiwa vimeanza kuharibiwa kutokana na Mabadiliko ya tabianchi.

Mahojiano na wananchi kisiwa cha Jibondo:

Baadhi ya wananchi wa kisiwa cha Jibondo ambapo wameeleza kuwa kisiwa hicho kimeanza kulika katika baadhi ya maeneo kwani kwa sasa maji yameweza kuingia katika ardhi.

Kwa mujibu wa wakazi wa Jibondo ambapo maana ya jina hilo ni jiwe kubwa na ndivyo kilivyo kisiwa hicho, kwani kipo juu ya mwamba mkubwa kwa sasa baadhi ya maeneo maji ya bahari yameingia baharini.

Zahoro Swed mkazi wa Jibondo amemweleza mwandishi wa habari hizi kuwa, awali katika eneo wanaposhushia vyombo vya usafiri lilikuwa mbali na majini, lakini sasa eneo hilo limemezwa na maji yamesogea zaidi.

Kwa upande wa wananchi wa kisiwa cha Chole ambacho ni kisiwa kidogo na ndio kisiwa chenye utalii na urithi wa kale ikiwemo magofu na majumba ya zamani, wananchi wengi wa kisiwa hicho wamelalamikia juu ya elimu ndogo ya Mazingira kutolewa licha ya kuihitaji mara kwa mara.

Wakazi hao wa kisiwa hicho walipaza sauti kwa kueleza kuwa, wengi wao wanajishughulisha na shughuli za baharini ikiwemo uvuvi na suala la kilimo cha mwani ambapo wamekuwa wakishuhudia matatizo ya kimazingira yanayotokea baharini mara kwa mara.

Swaumu Mohammed ambaye ni mkazi wa kisiwa hicho cha Chole anayefanya shughuli za kilimo cha zao la mwani anaeleza kuwa wamekuwa wakishuhudia mabadiliko kadhaa ndani ya bahari hiyo ikiwemo baadhi ya maeneo kuwa tofauti na awali.

Hivyo elimu zaidi inahitajika katika kujua mabadiliko ya tabianchi ni yapi na namna ya kujikinga nayo hasa sisi tunaoshinda baharini muda mrefu” alieleza Bi. Swaumu alipoulizwa kama anafahamu juu ya hali ya mabadiliko ya tabianchi ama .

Mbali na wananchi wa visiwa hivyo, kwa upande wa wananchi wa Kisiwa cha Bwejuu kwa upande wao wameonyesha wasiwasi wao kuwa baadhi ya maeneo yanayozunguka kisiwa hicho yamekuwa yakiliwa na maji kwa muda mrefu huku kukiwa hakuna juhudi za haraka kunusuru hali hiyo.

Wananchi hao wameonyeshwa kusikitishwa na kasi ya hali hiyo kwani imekuwa ikiongezeka mara kwa mara na hakuna hatua ya haraka iliyochukuliwa.

Viongozi wa Serikali wa  Kisiwa hicho cha Mafia, wamebainisha kuwa, karibu visiwa vyote vinavyokaliwa na watu wamekuwa wakijitahidi kufikisha elimu mbalimbali huku akisisitiza wito wa wadau binafsi kujitokeza kusaidia na serikali katika swala hilo la utoaji wa elimu ya Mazingira na mabadiliko ya tabianchi hasa katika kukabiliana na majanga yatokanayo na masuala hayo.


DSC_2442
Moja ya vyombo vya uvuvi na usafirishaji abiria vikiwa vimepaki katika fukwe za Kisiwa cha Chole huku vikisubiria maji kurejea katika eneo hilo kama vilivyokutwa na mwandishi wa makala haya. (Andrew Chale).
DSC_2431
DSC_2412
Pichani ni katika eneo la Fukwe za Wavuvi kama linavyoonekana lilivyoharibika kulikosababishwa na mabadiliko ya tabianchi. Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo la Kilindoni wameeleza kuwa, miaka ya nyuma hapo palikuwa na minazi huku maji ya bahari yakiwa mbali, lakini kwa kadri mabadiliko yalivyotokea, eneo hilo limeweza kuliwa na kufanya minazi kupotea hali iliyosababisha kuweka mfereji/mto mdogo ambao unapitisha maji kutoka baharini na kuchanganyika na yale ya mvua ya kwenye makazi ya watu. (Picha na Andrew Chale)
DSC_2441
Taswira ya kisiwa cha Chole kinavyoonekana..
26228_381332445043_739925_n
Baadhi ya fukwe za kupendeza za kisiwani Mafia zinavyookena kwa picha hii iliyopigwa juu
01TMFI-IM1001-mafia-island-lodge-1475
331279_10150264327085044_7660323_o
Moja ya sehemu za eneo la Kisiwa cha Jibondo kama inavyoonekana pichani ambapo kisiwa hicho kipo juu ya mwamba ama jiwe kama inavyofahamika Jibondo ama jiwe kubwa. (Picha ya kwa hisani ya Mafia Island page ya fb).
DSC_2597
Pichani Mwandishi wa Makala haya akiwa katika boto maalum kwa safari za visiwa vilivyo ndani ya Mafia ambavyo Kisiwa hicho kinakadiliwa kuwa na Visiwa vidogovidogo zaidi ya vitano. Picha ya chini Mwandishi akiwa katika Kibao cha Shule ya Kijiji cha Chole katika Kisiwa cha Chole ambacho ni kisiwa pekee chenye magofu ya Kale na vitu vya thamani vya enzi za zamani vikiwa vimehifadhiwa huko.
DSC_2521
Kisiwa cha Chole
visiwa vya mafia ndani ya mafia
Moja ya visiwa vidogo na vya kuvutia ndani ya Kisiwa cha Mafia.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.