MTANGAZAJI

MAHAFALI YA NANE YA CHUO KIKUU CHA ARUSHA (UOA) YALIVYOFANA

Katibu mwenza wa Makao makuu ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Ulimwenguni Dr Rosa Taylor Banks

Makamu Mkuu wa Chuo Profesa Emanueli Matiku (Kulia)akihutubia

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Katibu mwenza wa Makao makuu ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Ulimwenguni Dr Rosa Taylor Banks amewataka wahitimu wa vyuo vikuu kuwa wavumilivu ili kufikia malengo ya mafanikio maishani.

Akizungumza kwenye mahafali ya nane ya Chuo Kikuu cha Arusha  jana Novemba 30 mwaka huu, Dr Banks ambaye alikuwa mgeni rasmi amesema uvumilivu ni zaidi ya kuwa na elimu,ubunifu,madaraka na utajiri kwani watu wote walio na mafanikio walipitia changamoto mbalimbali lakini walikabiliana nazo kwa kuwa wavumilivu na kusonga mbele bila kukata tamaa.

Awali akihutubia mamia ya watu waliohudhuria mahafali hiyo chuoni hapo Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Arusha Profesa Emanueli Matiku amesema Chuo hicho sasa kina mkakati wa kuanzisha kitivo cha sayansi ya jamii na teknolojia ili kukidhi mahitaji ya jamii ya kitanzania na kuwezesha kupata wanafunzi wengi wanaojiunga na chuo hicho kutokana na mkazo uliotolewa na serikali ya Tanzania katika kuandaa wataalamu wa fani mbalimbali za sayansi.

Jumla ya wahitimu 792 walitunukiwa stashahada,shahada za uzamili na shahada katika fani za elimu,dini,,usimamizi wa fedha,usimamizi wa biashara na thiolojia .

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.