MTANGAZAJI

MOROGORO:KONFERENSI YA MASHARIKI MWA TANZANIA (ETC) YA WAADVENTISTA WASABATO SASA KUGAWANYWA


Tume ya Divisheni ya Africa Mashariki na Kati ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato leo imetangaza kuridhishwa na kuigawa konferensi ya mashariki mwa Tanzania ETC kuwa koference mbili na kukipa hadhi Kiwanda cha Uchapaji (TAP) kuwa nyumba ya uchapaji.
Mwenyekiti wa Union ya Kusini mwa Tanzania Mch Magulilo Mwakalonge amesema kuwa tume imetathimini uwezekano wa kugawa ETC kuwa Konferensi mbili yaani  konferensi ya Mashariki na Kati mwa Tanzania na Konferensi ya Kusini Mashariki mwa Tanzania na TAP kupewa hadhi ya kuwa nyumba ya uchapaji.     
 Mchungaji Mwakalonge amesema kuwa kazi iliyobaki ni tume kupeleka pendekezo na hati katika kamati ya division, na kinachosubiliwa ni maamuzi ya kamati ya division ambapo hivi karibuni tume hiyo iliyokuja kutoka nairobi yalipo makao makuu ya divisheni hiyo ilikuwa na wajumbe watano.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.