DAR ES SALAAM:SERIKALI YAWATAKA WAIMBAJI WA KWAYA ZA WAADVENTISTA WASABATO KUSAJILI NYIMBO ZAO BARAZA LA SANAA LA TAIFA
Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Angellah Kairuki akihutumia katika uzinduzi huo |
Naibu
Waziri wa sheria na katiba Anjela Kairuki amezitaka kwaya za makanisa ya Waadiventista Wa Sabato nchini Tanzania kusajili matoleo ya nyimbo wanazoimba kwa Baraza
la Sanaa la Taifa (BASATA) ili kupata fursa mbalimbali kutoka serikalini.
Agizo
hilo amelitoa hapo jana katika uzinduzi wa toleo la sita la video ya waimbaji
wa kwaya ya Kanisa la Waadivestista Wa Sabato Kurasini inayoitwa Tufundishe Kuabudu uliofanyika katika viwanja vya maonesho ya sabasaba jijini Dar-es-saalam.
Angellah
Kairuki amesema kuwa kwaya zinapaswa kusajili nyimbo zake basata ili kuweza
kunufaika kiuchumi kutoka katika mamlaka mbalimbali za serikali ikiwemo zinazowezesha
wananchi kiuchumi.
Amesema
serikali itaendelea kuwasaidia wasanii mbalimbali zikiwemo kwaya katika kupata
miundo mbinu mbalimbali ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na hilo litafanyika
iwapo kwaya hizo zitakuwa zinatambuliwa kupitia BASATA na Wizara ya Habari,Vijana Utamaduni na Michezo.
Uzinduzi huo ulioshuhudiwa na mamia ya wakazi wa jiji na Dar es salaam uliwakutanisha waimbaji wa Mbiu kwaya,Mburahati,Nyegezi,light
beares,Royal Advent ,Vocapella,KKKT Keko,Namsifu Mbuso na Masalio Echoes toka Nairobi
nchini Kenya.
Post a Comment