MTANGAZAJI

TABORA:WAALIMU WAAGIZWA KUFUATILIA MAHUDHURIO YA WATOTO SHULENI



Mwenyekiti  wa halmashauri ya wilaya ya Sikonge mkoani Tabora Robert Kamoga amewaagizi  waalimu wakuu wa shule zote za msingi katika wilaya hiyo kuhakikisha wanafuatilia mahudhurio ya watoto shuleni,ili kubaini watoto wasiofika shuleni  ili wazazi wao wakamatwe mara  moja na kutozwa faini.

Kamoga ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya siku ya kupinga utumikishwaji  kwa watoto iliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Udongo kata ya Ipole wilayani  Sikonge mkoani Tabora.

Sambamba na hilo amewaagiza watendaji wote wa halmashauri hiyo kuanzia ngazi ya vijiji na kata kuwachukulia hatua kali watu wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya utumikishwaji watoto katika maeneo yao .

Kamoga amepongeza jitihada zinazofanywa na mradi wa PROSPER katika kutokomeza utumikishwaji watoto kwenye shughuli za kilimo katika wilaya hiyo.

Tabora ni miongoni mwa mikoa 5 inayoelezwa kuwa inaongoza kwa umaskini hapa nchini na asilimia kubwa ya wananchi wake ni maskini hali inayochangia watoto wengi kutumikishwa katika kazi ngumu kwa ujira mdogo.

Sheria ya mtoto na.21 ya mwaka 2009 kifungu cha 78 (1)
inakataza mtu yeyote kuajiri au kutumikisha watoto katika shughuli
yoyote ile inayowaathiri watoto.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.