MTANGAZAJI

MOSHI:WAKAZI WAHOFIA KUWEPO KWA UGONJWA WA DENGUE



Hofu imetanda kwa wakazi wa Manispaa ya ya Moshi mkoani Kilimanjaro  wakihofia kuumwa na mbu anayeeneza ugonjwa wa dengue baada ya watu watano kugundulika kuumwa na wengine 11 wakionesha dalili za ugonjwa huo.


Kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Dr Christopher Mtamakaya ameyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ugonjwa dengue na kutoa tahadhari  kwa wananchi kufanya usafi katika mazingira yao ili kuepuka mazalia ya mbu.


Dr mtamakaya ambaye pia ni mganga mkuu wa manispaa hiyo amesema watu watatu wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya mawenzi  na wengine watatu wakiwa wamelazwa katika zahanati.


Amesema  sampuli za ugonjwa huo zinachukuliwa ili kujua kama ni  ugonjwa hatari wa  dengue licha ya kuonesha dalili zote za ugonjwa huo.


Amesema tayari ugonjwa huo upo mjini  humo na  kwamba uwezekano wa kuambukizwa ni mkubwa  na amewashauri wananchi kuchukua tahadhari




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.