MTANGAZAJI

MWANAMKE MJAMZITO HUKO SUDAN AHUKUMIWA KUNYONGWA BAADA YA KUBADILI DINI NA KUWA MKRISTO



 
(picha toka Sky News)
Mahakama ya Sudan imemhukumu mwanamke mjamzito adhabu ya kunyongwa baada ya kubadili dini na kuwa mkristo.

Tovuti ya shirika la habari la Sky News hii leo imemtaja mwanamke huyo kuwa ni Mariam Yahya(27) ambaye alikamatwa pamoja na mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miezi 20 na aliamuliwa kuikana Imani yake na kurudi katika dini ya kiislamu.

Pia ameshitakiwa kwa kosa la kuolewa na mwanamme mkristo.
Adhabu hiyo ya kifo ilitolewa japo kuwa barozi za mataifa ya magharibi ziliomba uhuru wa kuabudu uheshimiwe.

Katika Mahakama ya Khartoum Jaji Abbas Al Khalifa alisema “Tulikupa siku tatu za kuacha uamuzi wako lakini ukasisitiza kutorudi katika uislamu,ninakuhukumu kunyongwa”

Mwanamke huyo aliyezaliwa na mwanamke mwislamu alihukumiwa katika sharia za kiislamu ambayo ilipitishwa kwa lazima nchini Sudan mwaka 1983.

Mariam Yahya ameolewa na mkristo raia wa Sudani ya Kusini ambayo ilipata uhuru wake mwaka 2011 baada ya vita vya wenyewe.

Kabla ya hukumu hiyo viongozi wa dini ya kiislamu walizungumza na mwanamke huyo kwa muda wa dakika 30 wakimshawishi kurudi katika Imani yake ya kwanza na alimwambia jaji kuwa  yeye ni mkristo.

Kufuatia adhabu hiyo mmoja wa wanasheria wake Mohanad Mustafa amesema atatafuta njia ya kukata rufaa kuhusu hukumu hiyo.

Jumla ya watu 100 miongoni mwao wakiwa ni wawakilishi wa barozi mbalimbali za mataifa ya magharibi ambayo ni Marekani,Canada na Uholanzi walihudhuria mahakamani hapo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.