MTANGAZAJI

WAKAZI WA TABATA DAR ES SALAAM WAKERWA NA TANESCO KUTOWAPATIA UMEME



Wakazi wa Tabata Kisiwani jijini Dar-es-saalam wamekerwa na kitendo cha kuachwa na shirika la ugawaji wa umeme nchini Tanesco katika hali ya wasiwasi na giza kila uingiapo usiku kwa zaidi ya wiki moja sasa baada ya Tanesco kukata umeme katika eneo hilo .


Kutokana na nguzo ya umeme kuangukia moja ya nyumba na nyaya zake kushuka chini kiasi cha kuchezewa na watoto  huku wakidai kuwa shirika hilo halijarejea kuresha huduma hiyo .


Edward Luoga ambaye ni mkazi wa eneo hilo anasema kuwa matatizo haya yametokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha  chini kwa wingi khali inayosababbisha uharibifu wa miundombinu hiyo.


Amesema  nguzo iliyoanguka katika maeneo hayo ni miongoni mwa vyanzo vya matatizo ya nishati hiyo  ya umeme  katika eneo hilo.


Wakazi hao wamesema tangu shirika hilo lifike katika eneo la tukio na kuona yaliyojiri lilikata huduma hiyo na hivyo kupelekea changamoto kubwa ya huduma hiyo kwa maeneo hayo jijini.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.