MTANGAZAJI

MELI ILIYOKUWA NA ABIRIA 460 YAZAMA KATIKA PWANI YA KOREA YA KUSINI



Oparesheni ya uokozi inaendelea kufuatia ishara za dharura zilizoripotiwa kutokana na  meli moja iliyobeba takriban abiria 460 katika pwani ya Korea Kusini kuzama.

Maafisa wanasema kuwa walinzi wa pwani hiyo wanatumia, meli za wanamaji wa Korea pamoja na ndege za uokoaji kuwaokoa watu waliokuwa katika meli hiyo.ambapo abiria 160 wameokolewa na wengine wakishauriwa kuruka baharini ili waokolewe.

Meli hiyo ilikuwa imebeba idadi kubwa ya wanafunzi ikitoka Incheon iliyoko kwenye visiwa vya kifahari vya Jeju .

Shughuli ya uokoaji bado inaendelea na walioshuhudia ajali wanasema kulisikika kishindo kikubwa kabla ya ferry hiyo kuanza kuzama zaidi ya kilomita 20 kutoka ufukweni.
Chanzo:BBC

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.