MTANGAZAJI

BIASHARA YA NGONO,KUJAMIANA KINYUME NA MAUMBILE VIKWAZO KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI



Kushamiri kwa biashara ya ngono katika maeneno ya mijini,tabia ya kujamiana kinyume na maumbile na matumizi ya dawa ya kulevya imetajwa kuwa ni vikwazo vikubwa katika mapambano  dhidi ya UKIMWI.

Licha ya kasi ya maambuzi ya  virusi vya ugonjwa huo kupungua kutoka asilimia saba mwaka 2003 hadi asilimia 5.1 mwishoni mwa mwaka juzi  lakini takwimu za kitaifa zinaonesha kuwa kwa watu walioko katika makundi hayo maambukizi yamefikia hadi asilimia 40.

Taarifa hiyo imetolewa  katika washa ya siku mbili iliyoendeshwa na tume ya taifa ya kudhibiti UKIMWI nchini Tanzania (TACAIDS) kwa ajili ya kusambaza mkakati wa tatu kwa wadau mbalimbali kutoka katika mikoa ya Tabora Shinyanga,Simiyu na wenyeji Singida.

Pamoja na mambo mengine yaliyoanishwa katika mkakati huo,msisitizo mkubwa wa Maofisa wa  TACAIDS kwa  halmashauri nchini kuelekeza nguvu zao kwa  makundi maalum.

Mapendekezo ya wadau katika kukabiliana na tatizo ni kurekebisha sheria zilizopo na kutoa elimu zaidi kwa jamii.

Usambazaji wa mkakati wa tatu wa Taifa kwa ajili ya kudhibiti Ukimwi nchini Tanzania ,unalenga kupunguza kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo hadi kufikia asilimia 0.16 ifikapo mwaka 2018.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.