MTANGAZAJI

IDADI YA WAGONJWA WA KIFUA KIKUU JIJINI ARUSHA YAONGEZEKA

Idadi ya wagonjwa wa kifua kikuu jijini Arusha,Tanzania  imepanda kwa asilimia 7.5 kwa mwaka 2012-2013.Ongezeko hili linatokana na juhudi kubwa zilizopo kati  wadau mbalimbali wa kupambana na ugopjwa huu katika kuweka wazi kwa kutoa Elimu inayohusu jinsi ya kujikinga na tiba ya kifua kikuu.

 Akizungumza ofisini kwake mapema jana,mratibu wa mapambano dhidi ya ugojwa huu jijini jijinii Arusha Maiko Kingazi ameeleza kuwa jamii imehamasika vya kutosha katika kutoa taarifa ya wenye dalili na uelewa juu ya ugonjwa huu imeongezeka kutokana na Elimu inayotolewa na wadau mbalimbali kwa jamii.

Tangu awali ulikuwepo ugonjwa huu tatizo lilikuwa kuwapata na kuwatambua waliopata maambukizi ya kifua kikuu jambo ambalo kwa sasa wananchi wana uelewa mpana hivyo wana jitokeza katika kupima ili kubaini wameambukizwa au laa.

 Aidha kwa upande wake mratibu wa mapambano dhidi ya kifua kikuu  na ukoma jiji la arusha kanda ya Magharibi Dr Lameki Kaaya amezitaja changamoto zinazoikabili ofisi yake katika kupambana na ugonjwa wa kifua kikuu mojawapo ikiwa ni kuhama kwa wagonjwa,ambayo husababishwa na wagonjwa wanaokuja kujtibiwa kutokt mikoani kutomaliza matibabu kutokana na unyanyapaa unaojitokeza kwa ndugu na jamaa wanapogundua kuwa ndugu yao ameshapata maambukizi.
            
 Hata hivyo Dr Kaaya alitoa wito kwa jamii na wananchi kwa ujumla kuwa na mazoea ya kupima afya zao mara kwa mara ili kuweza kubaini tatizo mapema na kushughulikiwa kwa wakati.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.