MORNING STAR TELEVISHENI YAPATA KIBALI CHA KURUSHA MATANGAZO

Mkurugenzi
 wa Vyombo vya Habari wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania 
Mchungaji Musa Mika (pichani) jana mchana  kupitia radio  ya Morning star
 ametangaza rasmi kuwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeipa 
Kanisa hiyo kibali cha kurusha matangazo ya Televisheni tarajiwa ya 
Morning Star.
Mchungaji
 Musa Mika pia amesema uzinduzi wa Morning Star Televisheni utafanyika 
hivi karibuni na wakati ukifika watatangaza king'amuzi kitachokuwa 
kinarusha matangazo ya kituo hicho kinachomilikiwa na Kanisa la 
Waadventista wa Sabato Tanzania.
Mchungaji 
Mika pia alichukuwa fursa hiyo kwa kuwashukuru waumini wa kanisa hilo, 
wapenzi wa radio ya Morning Star na watanzania wote kwa ujumla kwa kuwa 
pamoja nao katika sala kwa muda mrefu wakati wakisubiri habari njema 
kama hii.
Chanzo:chingaone 

Post a Comment