KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO LATOA MSAADA KWA WAFUGAJI WALIOCHOMEWA NYUMBA
Mchungaji Alphonce Mayo akikabidhi magunia ya vyakula kwa waathirika wa moto |
Moja ya nyumba zilizoteketea
Mchungaji Mayo akimwaangalia mtoto aliyekuwa anaumwa, katika moja ya nyumba zilizoathirika na moto |
Askofu Mkuu
wa kanisa la Wa-Adventista wa Sabato, Jimbo la Kaskazini-Mashariki mwa
Tanzania (NETC) Mchungaji Alphonce Mayo, jumatano hii ametoa msaada kwa niaba ya
jimbo la kaskazini mashariki mwa Tanzania kwa nyumba 16 zilizochomwa
moto wafugaji wa kimasai
Tukio hili la kuchomwa nyumba za wafugaji limeleta hasara kubwa
ya Nyumba 16, Mifugo, Vyombo, baiskeli, viti, Nguo kwa nyumba 16 za
wafugaji, na kati ya nyumba hizo 12 ni za waumini wa kanisa la
Waadventista wa Sabato, wanaosali katika kundi la Chang’andu-Mtaa wa
Handeni,Tanga.
Msaada huo ni madebe 24 ya unga wa mahindi,
madebe 24 ya Mahindi, kilo 100 za Maharage, Maturubali ya mahema 10.
Katika hotuba yake ya kuwatia moyo baada ya kushuhudia nyumba
zilizochomwa moto, Mchungaji Mayo alisema, katika Biblia uko mfano wa Ayubu
ambaye alipatwa na majanga makubwa na mazito ya kupotelewa na watoto
pamoja na vitu alivyokuwa navyo lakini kamwe hakumuacha Mungu.
Mayo aliwasihi wahanga hao waendelee kumtegemea Mungu hasa katika wakati huu
mgumu, kwa kudumu katika maombi na ibada bila kulipa kisasi.
Akihitimisha hotuba yake Mchungaji Mayo ameyaomba makanisa ya WaAdventista
jimbo la kaskazini mashariki, kukusanya misaada mbalimbali ya
vyakula, nguo, mahema, ili kuwasaidia ndugu zetu hawa, ameomba misaada
hiyo ipitie kwa wachungaji wa mitaa katika mitaa 37 ya jimbo hilo, ili
iwafikie wahanga hao.
Naye mchungaji Kiongozi wa mtaa wa Handeni Mchungaji Wilbert Sambeke pamoja na Kaimu mwenyekiti wa kijiji hicho, wameshukuru kwa kanisa kutoa msaada huo kwani wananchi hao wapo katika shida ya kukosa mahitaji yao muhimu hasa wakati huu ambapo
mvua zinaendelea kunyesha kwa wingi katika eneo hilo
Tukio hili la kusikitisha
lilitokea usiku wa kuamkia Alhamis machi 28,2013 saa nne
usiku katika kijiji cha Chang’andu, Mombo wilaya ya Korogwe, kwa
kundi kubwa la watu wanaotuhumiwa kuvamia kwa sababu za uhasama wa wafugaji na
wakulima.
Post a Comment