MTANGAZAJI

USO KWA USO NA WAZIRI MKUU WA TANZANIA KUPITIA STAR TV

Mh Waziri MKuu wa Tanzania  Mizengo Pinda akifanya mahojiano na Baraka Baraka nchi Uingereza
Salam,
Urban Pulse Creative wakishirikiana na Star tv wanakuletea Mahojiano Maalum na Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipofanya ziara nchini Uingereza hivi karibuni. Mahojiano haya yalikuwa yamelenga zaidi kupata ufahamu na uchambuzi wa namna serikali yetu ya Tanzania inavyofanya kazi pamoja na changamoto zake.
 
Mbali na hapo tulijadiliana kuhusu Majukumu ya Waziri mkuu, Chakula, Nishati, Jumuiya ya Afrika Mashariki na mchakato wa katiba Mpya kuelekea kuazimisha miaka 50 ya uhuru.
 
Mahojiano haya yalifanywa na Baraka Baraka  Kutoka Urban Pulse na yatarushwa Hewani kupitia  kituo cha Star TV Jumapili ijayo Tarehe 30 octoba 2011 kuanzia saa 10.30 katika kipindi cha Medani za siasa.
 
Tafadhali usikose kuangalia kipindi hiki ili upate kujifunza mambo mbalimbali kuhusu Tanzania na Serikali yetu.
 
Asanteni,
 
Frank Eyembe-Urban Pulse Creative

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.