MAMA GAGI APATA AJALI YA GARI
Jumamosi Juni 6,2009 haitasahaulika katika familia ya Mch Jacob Gagi ambaye Mwenyekiti wa Kanda ya Mashariki mwa Tanzania ya Kanisa la Waadventista Wasabato (ETC) baada ya mke wake kupata ajali katika eneo la Doma barabara ya Morogoro -Iringa iliyohusisha gari lake(pichani) na gari la Mkuu wa Mkoa wa Rukwa .
Mama Gagi akiwa na Safi na watoto 9, wawili kati yao walijeruhiwa walikuwa wakielekea kanisani huko Doma kwa program maalum na gari la Mkuu wa mkoa wa Rukwa likuwa limemchukua ofisa tawala wa Mkoa na familia yake ambapo mtoto wao wa miezi saba alifariki papo hapo.
Akizungumza na blog hii leo mchana baada ya kutoka hospital Mama Gagi amesema hata haamini kuwa bado yu hai na watoto aliokuwa amewachukua maana anaina ni muujiza wa Mungu alionfanyia kwa kumponya katika ajali hiyo mbaya.
Post a Comment