MTANGAZAJI

JUMUIYA YA WATANZANIA WAISHIO DALLAS TEXAS, MAREKANI YAPATA UONGOZI MPYA

 


Katibu Mkuu Godfrey Mwamsoyo

Everest Michael, Mwenyekiti mpya.

 
Jocylne devosta mweka  Hazina.

Jumuia ya Watanzania waishio katika jiji la  Dallas,Texas Marekani  Tanzanians Dallas,Januari 12 mwaka huu imefanya mabadiliko ya uongozi kwa kuwachagua viongozi mpito watatu. Uchaguzi huo ulihudhuliwa watanzania waishio katika eneo hilo  na kufanya maamuzi ya uongozi wa dharura kutokana na kujiudhuru kwa uongozi uliyopita.

 

Watanzania katika jiji hilo la Dallas na vitongoji vyake wanaamini kwamba, mshikamano wao ambao ndio kilikuwa ni chanzo kikubwa cha wao kuwa kitu kimoja wakati wa misiba na dharura za aina yote kimaisha wanavyoishi ughabuni. Kufuatana na katiba ya jumuiya hiyo  kikao kiliteua  wagombea  wa mpito mpaka hapo mwezi Julai katika uchaguzi mkuu chini ya utaratibu  mpya.

 

Uongozi uliotumikia jumuiya hiyo kwa muda sasa na hatimae kujiudhuru kwa hiyari, ni mwenyekiti Bw. Benedict Kazora, Bi Maria Musomi, Makamo mwenyetkiti na  Katibu Bi Viola  Mbise. 

Maamuzi hayo ambayo yanaelezwa kuwa yalikuwa ya ghafla yaliwakilishwa kwenye kamati ya ushauri na kutangazwa rasmi katika tofuti za mitandao ya kijamii mara moja. Harakati zipo mbioni kuwasiliana na uongozi uliopita kukabidhiana nyaraka na uongozi mpya mpito haraka iwezekanovyo.

 

Jumuiya hiyo, imewachagua viongozi wake mpito wapya kupitia utaratibu wa kuwapigia kura wale wote walioteuliwa na wanajumuiya baada ya mkutano huo mahususi  kuziba hizo nafasi hizo. 

Waliochaguliwa ni Mwenyekiti ni Bw. Everest M. Michael, Katibu Bw. Godfrey Mwamsoyo na mweka hazina ni Bi Jocyline Vadesto. 


1 comment

Anonymous said...

Habari! Samahani nilikuwa naomba mawasiliano ya Jumuiya ya watanzania waishio Dallas Texas, hapa marekani. Asante

Mtazamo News . Powered by Blogger.