DAR ES SALAAM:BENARD MEMBE ATAKA JUMUIA ZA KIMATAIFA KUWAJIBIKA KUHUSU AMANI
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam kushiriki katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. ( Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Jumuia ya Kimataifa imetakiwa kuwajibika kuhakikisha kwamba wanaweza kuwepo na amani na usalama kwa kuwa hilo ndilo tatizo kubwa duniani.
Hayo alisema Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard membe katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
Hafla hiyo imefanyika viwanja vya Mnazi Mmoja mapema zaidi kuliko tarehe iliyopaswa ya Oktoba 24 kutokana na Tanzania kuwa katika mchakato wa uchaguzi.
Waziri Membe alisema kwamba dunia kwa sasa ipo katika changamoto kubwa ya usalama kutokana na mizozo inayoendelea katika nchi kadhaa duniani.
Alisema kumekuwepo na wimbi kubwa la mapigano ndani ya nchi mbalimbali katika nchi mashariki ya kati, Ulaya na hata Afrika, kukua kwa ugaidi na siasa za kibaguzi.
“ Sote tunafahamu shida iliyopo katika nchi kama Syria, Iraq, Somalia, Libya, Afghanistan, Yemen na jamhuri ya Afrika Kati” alisema waziri Membe na kuongeza kuwa matukio ya vita ya mara kwa mara, misimamo mikali na ugaidi vimekuwa vikisababisha vifo vingi na mateso kwa jamii.
Pamoja na kuzungumzia haja ya amani kutokana na dunia sasa hivi kufikia kiwango cha juu cha wakimbizi ndani na nje ya nchi zao, Waziri Membe alihimiza mabadiliko katika uendeshaji wa Umoja huo ili kuleta uwiano wa uwajibikaji kimataifa.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akisalimiana na baadhi ya wakuu wa Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa nchini huku akiwa ameambatana na pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Liberata Mulamula (kushoto).
Gwaride maalum katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa likitoa heshima kwa mgeni rasmi Waziri Membe (hayupo pichani).
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akikagua gwaride maalum lililoandaliwa kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum akisoma dua kubariki sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
Kiongozi wa madhehebu ya Kikristo akiongoza sala katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
Meza kuu kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy, Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin William Mkapa pamoja na mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe wakishiriki sala maalum ya kuombea amani ya nchi na Umoja wa Mataifa.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akitoa hotuba katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe (kulia) akimpongeza Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin William Mkapa kwa hotuba nzuri aliyoitoa.
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mh. Bernard Membe tuzo ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa kwa kuzingatia mchango wake katika Maendeleo ya Milenia (MDGs) na Maendeleo Endelevu (SDGs) katika maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja huo jana katika viwanja vya Mnazi mmoja.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (katikati) akimpongeza Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe mara ya kukabidhiwa na Umoja wa Mataifa kwa kutambua mchango wake katika Maendeleo ya Milenia (MDGs) na Maendeleo Endelevu (SDGs) katika maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja huo jana katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar.
Mshehereshaji katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa ambaye pia Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Mindi Kasiga akifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja.
Meza kuu.
Mabalozi, Wakuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Wadau wa Maendeleo pamoja Viongozi wa Serikali wakiwa jukwaa kuu.
Wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mmoja wa viongozi wa madhehebu ya dini wakifuatilia jambo kwa umakini katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
Pichani juu na chini ni sehemu ya wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja Mataifa walioshiriki katika kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulida Hassan na Eliet Magogo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakibadilishana mawazo wakati wa sherehe hizo.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali nao walishiriki.
Maafisa wa jeshi nao walishiriki.
Meza kuu katika picha ya pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini.
Meza kuu katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini pamoja na wadau wa maendeleo.
Meza kuu katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule mbalimbali walioshiriki kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
Meza kuu katika picha ya pamoja na wakuu wa mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania.
Meza kuu katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa.
Meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na wanafunzi walioshika mabango ya malengo endelevu.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin William Mkapa wakiondoka kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akiteta jambo na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum wakati akiondoka kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Post a Comment