RAIS KIKWETE AAGA UMOJA WA MATAIFA (UN)

Zifuatazo ni baadhi ya picha zinazomwonyesha Mhe. Rais katika Matukio mbalimbali Moja wapo Zikiwa ni hafla ambayo Rais wa Marekani, Mhe Barack Obama aliiandaa kwaajili wa Viongozi Wakuu wa Nchi na Serikali waliohudhuria Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Picha kwa hisani ya Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa


Mhe. Rais Kikwete akiwa na Mhe. Sophia Simba, Katibu Mkuu Balozi Liberata Mulamula na mwanamitindo Flaviana Matata muda mfupi mara baada ya kulihutubia Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa


Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu wa Antigua na Barbuda Mhe. Gaston Alphonso Browne, wengine katika mazungumzo hayo ni Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, Mwakilishi wa kudumu wa Antigua na Barbuda, Balozi Walton Webson mwenye miwani myeusi na Mkurungezi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestin Mushy
Chanzo:Ikulu blog
Post a Comment