MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:TANESCO YATANGAZA KUKATIKA KWA UMEME JUMA NZIMA NCHINI


Shirika la umeme nchini (Tanesco), limetangaza nchi kuingia ‘gizani’ kwa juma zima kuanzia leo Septemba 7,2015  kutokana na kuzimwa kwa mitambo ya gesi inayozalisha umeme kutoka Songosongo na kuanza majaribio ya gesi ya Mtwara inayosafirishwa kuja Kinyerezi jijini Dar es salaam. 

Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Felchism Mramba, amewaambia waandishi wa habari hivi karibuni kuwa baada ya kutembelea mtambo wa Kinyerezi I, sasa Watanzania wategemee umeme wa uhakika baada ya kuanza kuzalisha umeme kwa gesi ya Mtwara.
  
Kwa mujibu wa Mramba, mikoa itakayoathirika ni yote inayopata umeme wa gridi ya Taifa ukiwamo Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Dodoma, Morogoro, Singida, Mwanza, Mara, Mbeya, Iringa, Tabora, Shinyanga, Manyara na Zanzibar.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC), Dk. James Materegeo, amesema mchakato wa kuchukua gesi kutoka mitambo ya Madimba mkoani Mtwara imekamilika juzi na kazi inayofanyika ni ya majaribio.
  
Amesema uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi ya Mtwara utaisaidia serikali kuokoa takribani Dola za Marekani bilioni moja kwa mwaka ambazo zilikuwa zinatumiwa kununua mafuta mazito ya kuzalisha umeme.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.