MTANGAZAJI

WANANCHI WA KILOSA WAMLALAMIKIA MKURUGENZI WA HALMASHAURI



Wananchi katika baadhi ya vijiji vya wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro wamelalamikia Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndugu Masalu Mayaya kwa madai ya kutotekeleza wajibu wake katika kusimamia maendeleo ya sekta ya Afya.

Wananchi hao wametoa malalamiko hayo kufuatia kuwapo  kwa madai  kuwa hospitali  ya wilaya ya hiyo  imetelekezwa na hivyo kukosekana kwa huduma muhimu vikiwemo vifa tiba na dawa.

Wananchi hao wamesema kuwa kukosekana kwa huduma bora za afya katika hospitali hiyo  ya wilaya  kumesababishwa na mkururgenzi  huyo  kutokemea matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya umma.

Kwa upande wake  mkurugenzi huyo amesema tayari ofisi yake imeanza kufuatilia maagizo ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya  Ameir Mbaraka kuhusu fedha za miradi ya jamii zilizotengwa mwaka jana.

Amesema haoni sababu za yeye kulaumiwa na kupigiwa kelele  kama aliyefanya uhalifu badala yake wananchi wanapaswa kuzingatia  ukweli kuwa  huduma za afya katika hospitali ya wilaya ni changamoto zinazohitaji kufanyiwa kazi na kuwa hakuna matatizo makubwa.

Mayaya ameongeza kusema kuwa  jamii inapaswa kutambua majukumu yake ya halmashauri  pamoja na kuacha tabia ya kuwaingiza watendaji katika tuhuma za ubadhilifu na  ufisadi ,badala yake wawe na subira kuona jinsi wanavyoshughulikia  matatizo yanayokabili sekta hiyo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.