MTANGAZAJI

UPUNGUFU WA MAJI JIJINI MWANZA

Maadhimisho ya siku ishirini na sita ya wiki ya maji yameingia siku ya tatu leo huku wakazi wa maeneo ya ibanda,Buswelu Kabuhoro na Kiseke jijijni Mwanza. wakiwa hawana huduma ya maji.

Mamlaka ya maji safi na maji taka jijini mwanza MWAUWASA Imesema kuwa imefanikiwa kutandaza mabomba ya maji safi yenye urefu wa kilometa mia sita wakati kuna matanki saba ya maji yenye ujazo wa mita elfu thelethini na tatu 33,000.

Naye mkurugenzi mtendaji wa MWAUWASA Anton Sanga amesema kuwa watapunguza tatizo la maji katika maeneo yenye miinuko huku kauli mbiu ya maadhimisho ya maji mwaka huu ni uhakika wa maji na nishati


Maadhimisho ya hayo kimataifa yanafanyika Tokyo nchini Japan na yanatarajia kufikia kilele machi 22 mwaka huu nchini humo.


Na:Conges Mramba

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.