MTANGAZAJI

WAOSHA KUCHA NA MIGUU WANAVYOINGIZWA KATIKA HATARI YA KUAMBUKIZWA VVU



Utengenezaji wa kucha na uoshaji miguu ni biashara inayoku­wa kwa kasi hasa maeneo ya mijini ambapo wanawake wengi wana­husudu na kujihusisha na masuala ya urembo. 

Biashara hii inazidi kukua huku pia huduma zinazotolewa zikizidi kuongezeka kila kukicha, ambapo mara nyingi wanaotengeneza ku­cha, hujihusisha na usuguaji wa miguu, uchoraji wa tattoo ukandaji wa mwili (massage)na nyingine zi­nazofana na hizo. 

Kazi hii imetokea kuwa chanzo kimojawapo cha mapato na ajira mpya kwa vijana wengi hasa wa kiume, wenye umri wa miaka 17 hadi 35. 

Hata hivyo, uchuguzi uliofanywa na gazeti la mwananchi hasa jijini Dar es Sa­laam, umegundua kuwa vijana wen­gi wanaofanya biashara hii huishia kufanya ngono na wateja wao hasa wanawake wenye umri mkubwa na wa kati (Mijimama), ambao wame­wahi kuwahudumia zaidi ya mara moja, hivyo kutumbukia katika ha­tari ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa na Virusi Vya Ukimwi(VVU). 

Kwa mujibu wa takwimu za Ukimwi nchini, vijana wengi walio kwenye umri kati ya miaka 17 hadi 35 ndilo kundi linalotajwa kuwa ka­tika hatari kubwa ya kupata maam­bukizi ya VVU.

Hatari hiyo inatokana na mazin­gira hatarishi wanayokutana nayo vijana hao wanapofanya shughuli zao na kufanya vitendo hivyo kwa makusudi, wakati mwingine kwa kushawishiwa. 

 Uchunguzi una­onyesha kuwa wakati wa ufanyaji wa shughuli hiyo, hutokea baadhi ya wanawake wakaoshwa au kusugu­liwa sehemu za miguu zinazokaribia maeneo ya mapaja, hivyo kuam­sha hisia kati ya mtoa huduma na mpokea huduma. 
 
Hatua hiyo inatajwa kuwasaba­bashia baadhi yao kufanya ngono ambayo mara nyingi siyo salama, wanapotoa huduma katika maeneo tulivu ikiwamo saluni maalumu na nyumbani kwa wateja. 


Mmoja wa wafanyabiashara hiyo katika Soko la Mwenge Hamis Shaban(19) (siyo jina halisi) anase­ma kuwa kuna wakati wamekuwa wakiingizwa katika mtego na wateja.
Yule sista amenifanyia vituko muda mrefu, nikaona asije kunitangazia vibaya bure kwamba mimi siyo mwanaume kamili; hivyo kumwonyesha kuwa nimekamilika, nikalazimika kufanya, ingawa sasa hivi unavyoniuliza naanza kupata wasiwasi. 

Anasema kuwa hali hiyo hutokea mara nyingi hasa mteja anapotaka kwenda kuhudumiwa nyumbani kwake, ambapo hukuta tayari wameandaa mazingira, ambayo mwisho wake huishia katika hatua hiyo. 
 
“Mimi mwenyewe imenitokea siku chache zilizopita; kuna binti fulani amekuwa mteja wangu kwa muda mrefu, amekuwa akinifanyia vituko vya hapa na pale. Nilikuwa sijali, ila majuzi akaniambia niende kwake nikamchore tattoo,”anasema Shaban na kuongeza: 


“Eneo alilotaka nimchore ndilo lilianza kunipa wasiwasi, lakini kwa sababu ya pesa nikapiga moyo konde. Akavua blauzi yake na ku­taka nimchore kwenye titi; nilijari­bu kutimiza wajibu wangu, lakini mambo ambayo alikuwa akifanya, yalinisababishia uzalendo kunishin­da, hatimaye tukajikuta tukifanya ngono.”
  
Anafafanua kuwa sababu ny­ingine iliyosababisha kufanya ngono ilikuwa kutaka kujenga heshima kwa mteja wake huyo, ili amwone kuwa ni mwanaume aliyekamilika. 


“Yule sista amenifanyia vituko muda mrefu, nikaona asije kuni­tangazia vibaya bure kwamba mimi siyo mwanaume kamili; hivyo kumwonyesha kuwa nimekamilika, nikalazimika kufanya, ingawa sasa hivi unavyoniuliza naanza kupata wasiwasi.” 


Mahamod Abdalah anayefanya biashara hiyo eneo la Makumbusho, naye anakiri kuwepo na changamo­to mbalimbali, ambazo huwafanya wengi wao kuingia kwenye mitego na kufanya kazi ya kuwafurahisha wake za watu. 


“Hiyo changamoto kweli ipo, inahitaji moyo wa ziada kukabili­ana nayo. Wanakuja wanawake wa haja, utakuta anakufunilia maungo, anataka umsugue; yaani hatari tupu, sasa kama huna ujasiri, lazima utain­gia kwenye mtego.”


Chanzo:Gazeti la Mwananchi

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.