MASKINI NCHINI TANZANIA WANA WASIWASI NA ELIMU YA WATOTO WAO
Na:Mkama Mwijarubi
mtoto wa masikini kupata kwake elimu ni kwa kubahatisha, mzazi hana uwezo wa kumpeleka mtoto shule za binafsi zinazotoza ada kubwa anampeleka shule ya serikali ambapo anaamini ataweza kumuuhudumia, lakini ubora wa elimu anayoipata hapo mwisho wa siku haimpeleki kokote. Embu fikiria mtoto anaamka asubuhi ana kazi kibao za kufanya amalize akakimbizane na makondakta kwenye daladala akifika shule akakae chini kwani hakuna madawati darasani, darasa lina watoto mia moja hata pa kupulia hakuna, bado tunategemea mtoto huyo apate elimu bora???? serikali inajenga matabaka na inaendelea kujenga kwani haidhamini shulee za serikali kwa sababu watoto wao wanasoma nje ya nchi na shule binafsi, hawajali watoto wa masikini wapate elimu wasipate who care???
Post a Comment